Thursday, April 9, 2015

KLINIKI YA HUDUMA KWA WATEJA YA NSSF YAJAZA WATU TCC CHANG'OMBE

Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii limekuwa likiendesha Kliniki ya Huduma kwa Wateja katika viwanja vya TCC Chang'ombe kuanzia Tarehe 20 /03/2015 mpaka Tarehe 29/03/2015 ambapo huduma mbalimbali zimekuwa zikitolewa.

Huduma hizo ni pamoja na Kutoa Elimu kwa Wanachama na wasio Wanachama kuhusu mafao yapatikanayo kutoka NSSF, Kutoa Elimu ya miradi kama Viwanja Vilivyopimwa na Vyenye Huduma za maji, barabara na Umeme vya kiluvya, Nyumba za Kijichi awamu ya Tatu,  Pia wanachama waliweza kupata Taarifa za michango yao . Uandikishaji wa Wanachama wapya pia ulifanyika katika Viwanja hivyo.
 Akizungumza wakati alipotembelea banda hilo Mgeni Rasmi, Mkurugenzi Utamaduni kutoka wizara ya Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Prof. Herman Mwansoko aliisifia Kliniki hiyo ya NSSF kwa kuweza kuwa karibu na wateja lakini Pia alivutiwa na Teknolojia Mpya ya kuandikisha wateja kupitia kifaa cha TazPad ambacho kinaweza kuchukua taarifa zote za wanachama bila kuhitaji uwepo wa Kompyuta.

Kutokana na Umuhimu wa kuwafikia wanachama wetu, Kliniki hiyo itafanyika Tena siku ya Tarehe 12/04/2015 kwenye Viwanja hivyo vya TCC Chang'ombe.

No comments:

Post a Comment