Tuesday, March 31, 2015

Ugomvi wa watoto ulianzia kwenye chakula.. mmoja wao akachukua bastola



Hii ya leo inahusu tukio lililotokea huko Florida Marekani, ambapo mtoto mwenye umri wa miaka 13, amemshambulia kaka yake mwenye umri wa miaka 16 pamoja na mdogo wake mwenye umri wa miaka 6, kwa kuwapiga na risasi halafu akajipiga mwenyewe.
Polisi wamesema watoto hao walikuwa peke yao nyumbani kwao wakati mama yao akiwa kazini wakaanza kugombania chakula, mtoto huyo akachukua bastola na kuanza kuwashambulia wenzake, kaka yake alipiga simu Polisi  ambao walifika eneo la tukio na kumkimbiza Hospitali lakini mtoto aliyewapiga risasi pamoja na mdogo wake walikutwa wameshafariki.

 
Polisi wanafanya uchunguzi kujua jinsi mtoto huyo alivyoweza kupata silaha hiyo.

No comments:

Post a Comment